January 14, 2015

KIKOSI CHA VILLA SQUAD...

Uongozi wa Villa Squad umeliandikia barua Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), ukiomba mechi zao zilizobaki za Ligi Daraja la Kwanza zichezwe kwenye Uwanja wa Mabatini, Mlandizi unaomilikiwa na jeshi.

Hiyo ni baada ya kutokea fujo kwenye mechi yao dhidi ya Friends Rangers iliyochezwa wikiendi iliyopita kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam, uliomalizika kwa sare ya bao 1-1.

Ofisa Habari wa timu hiyo, Idd Godigodi, alisema kuwa, kutokana na fujo walizofanyiwa wachezaji na baadhi ya viongozi wao, basi hawataki kuutumia uwanja huo tena kwa hofu ya usalama wao.

Godigodi alisema tayari wameiandikia barua TFF kubadili uwanja huo na kuutumia huo wa jeshi kutokana na polisi wanaopangiwa kulinda usalama Karume kuonekana kuzidiwa na mashabiki wa timu mbalimbali wakiwemo wa Friends Rangers.

“Kutokana na fujo mbalimbali walizofanyiwa wachezaji wetu Nurdin (Bakari), Taita (Godfrey) na Redondo (Ramadhani Chombo), tumeona ni bora tubadili uwanja huu unaotumika kwa ajili ya mechi za ligi na tuhamie Mabatini Mlandizi.

“Kikubwa hatutaki kuona hiki kilichotokea kinaendelea kwa wachezaji na baadhi ya viongozi wetu wakifanyiwa fujo, hivyo tayari tumewaandikia barua TFF kwa ajili ya kuwafahamisha,” alisema Godigodi.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic