January 17, 2015


Kocha wa zamani wa Simba, Patrick Phiri, raia wa Zambia, amesema kuwa bado anaendelea na maisha mengine nje ya soka, ingawa yupo katika michakato ya kuhakikisha anapata timu ya kufundisha kwa kuwa soka ni sehemu ya maisha yake.


Kocha huyo mwenye rekodi ya kuchukua ubingwa wa Tanzania bila ya kupoteza mchezo wowote akiwa na kikosi cha Simba msimu wa mwaka 2009/2010, ‘alimwagwa’ na klabu hiyo mwishoni mwa mwaka jana kutokana na timu yake kutokuwa na matokeo mazuri katika michezo ya Ligi Kuu Bara.

Akizungumza kutoka jijini Lusaka, Zambia, Phiri aliweka wazi kuwa kwa sasa hana timu, anaendelea na majukumu mengine nje ya soka, lakini jitihada zinafanyika kupata klabu ya ‘kuikochi’ na hilo likikamilika kila kitu kitawekwa hadharani, huku akigoma kuelezea ishu ya malipo yake na Simba.

Mzambia huyo aliongeza kuwa, amefurahishwa na taarifa za Simba kubeba ubingwa wa Mapinduzi na anawapongeza kwa hilo, alisisitiza wana kikosi kizuri, hivyo wakicheza kwa umoja nyota yao itang’aa zaidi.

“Ninashukuru nipo na afya njema na ninaendelea na majukumu mengine nje ya soka, asante sana kwa kunikumbuka.

“Bado sina timu, tangu tuachane na Simba nilikuwa kwetu mjini Kitwe, lakini jana (juzi Alhamisi) nimerejea hapa Lusaka. Tunaendelea kufanya mipango ili kupata klabu ya kufundisha na tukifanikiwa katika hilo basi tutafahamishana.


“Nimesikia Simba wamepata ubingwa wa Mapinduzi, nimefurahi na ninawapongeza sana kwa hilo. Wana kikosi kizuri kama wakicheza kwa kujituma zaidi watapata mafanikio makubwa,” alisema Phiri huku akigoma kuzungumzia lolote kuhusu malipo yake na Klabu ya Simba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic