January 17, 2015


Kiungo na mshambuliaji wa zamani wa  Simba, Warundi, Amissi Tambwe na Pierre Kwizera, wanatarajia kuiburuza tumu hiyo Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuhusu madai yao ya kuvunja mkataba ambayo Simba haijawalipa.


Wachezaji hao walisitishiwa mikataba yao na kuahidiwa kulipwa, lakini wanasema hawajalipwa mpaka sasa, huku Tambwe akitua Yanga, Kwizera akirudi Burundi.


Tambwe amesema wamefikia hatua hiyo kutokana na kuchoshwa na uongo wa viongozi wa Simba dhidi yao kila wanapowasiliana nao.

“Hali hiyo imetuchosha na tunaona Simba siyo wakweli, Jumatatu ijayo (keshokutwa) tutapeleka malalamiko yetu TFF ili waweze kutusaidia kupata haki yetu.

“Wakati tunajiunga na timu hiyo walitupokea kwa mikono miwili lakini sasa hatuwaelewi kabisa jinsi wanavyotufanyia. Walipotuita kuwa wanataka kutuacha tulikubaliana nao vizuri, hivyo wanapaswa kuzingatia makubaliano hayo na siyo kutuzungusha,” alisema Tambwe.

Kila wanapoulizwa juu ya suala hilo, viongozi wa Simba wamekuwa wakijibu kwa ufupi kuwa wameshawalipa wachezaji hao.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic