January 11, 2015


Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van der Pluijm amesema wamejifunza mengi katika michuano ya Mapinduzi na yatawasaidia.


Pluijm raia wa Uholanzi amesema kumekuwa na mengi na yatawasaidia kwenye Ligi Kuu Bara na michuano ya Kombe la Shirikisho.

“Tumecheza michuano hiyo kwa mafanikio makubwa, kutolewa linaweza lisiwe jambo namba moja.
“Tumejifunza na kugundua matatizo kadhaa ya msingi ambayo tunayafanyia kazi. Kikubwa ni nini cha kufanya baada ya hapo.

“Tuna michuano ya ligi na ile ya kimataifa, hivyo lazima tujue tuna mzigo mkubwa mbele yetu,” alisema Pluijm.


Yanga ilitolewa katika hatua ya robo fainali ya Kombe la Mapinduzi huku ikiwa ndiyo timu inaongoza kwa kufunga mabao mengi na kuibuka na ushindi wa mabao manne mara mbili mfululizo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic