Unamkumbuka
yule straika aliyebatizwa jina la “bonge”, alikwenda kufanya mazoezi Yanga,
Kocha Marcio Maximo akamtosa, sasa yuko Hispania.
Suleiman Abdallah
Mbarouk amesema anaendelea vizuri katika klabu yake ya daraja la pili ua Jerez
ambayo imempeleka kwa mkopo Fosehill.
“Huku
naendelea vizuri kabisa, sasa nimerudi Uingereza kwa muda kwa ajili ya
mapumziko ya mwanzo wa msimu.
“Kitu ambacho
ninaweza kusema ni masikitiko yangu kuhusiana na yule aliyekuwa kocha wa Yanga,
(Marcio) Maximo. Alinifanyia kitu kibaya kwa kushindwa kunipa nafasi hata
kidogo kuonyesha uwezo wangu.
“Nilikuja
Yanga kufanya majaribio, lakini hakunipa nafasi hata kidogo. Badala yake
alionyesha hofu kama ningefanikiwa basi ningeweza kuwanyima nafasi ndugu zake
Wabrazil.
“Wanasema
mimi bonge, vipi nacheza Hispania, nacheza England? Kwani soka la England na
kwetu Afrika lipi lipo juu,” alisema.
“Nasikia
kafukuzwa, ila alinionea sana. Sasa nacheza kwenye timu yangu, nimecheza mechi
tisa, nimefunga mabao saba. Nitarudi Spain Januari 9 ili kuendelea na kazi.”
Mbarouk alifanya majaribio Yanga kwa siku moja
tu kabla ya Maximo kumzuia kuendelea kwa madai alikuwa na umbo kubwa.









0 COMMENTS:
Post a Comment