February 20, 2015

UONGOZI WA JUU WA SIMBA; MWENYEKITI EVANS AVEVA (KUSHOTO) NA MAKAMU WAKE, GEOFREY NYANGE 'KABURU'

Uongozi wa Simba pamoja umefikia uamuzi wa kumzuia mmoja wa viongozi wake kufika kambini kwa maslahi ya timu.


Taarifa za uhakika kutoka ndani ya Simba zimeeleza kiongozi huyo mwanandamizi, amezuiwa na tayari amepewa taarifa.

“Kweli kuna hatua zimechukuliwa na uongozi, tumeona kila anapokwenda linakuwa ni tatizo kubwa.

“Amekuwa akichangia kuwavuruga wachezaji, hivyo tulichoamua asiende kambini timu itakapokuwa Dar es Salaam au nje ya mkoa,” kilieleza chanzo na kuendelea:

“Mara kadhaa tumepata malalamiko, hata wachezaji wamekuwa wakilaumu sana kwamba anawachanganya na wakati mwingine anawaambia maneno ya kashfa, kitu kinachowavunja nguvu.

“Wachezaji pia wamelalamika amekuwa akiwapiga vita kwa kumwambia kocha kuwa wao hawafai lakini wanapokutana naye anawachekea.”

Hivi karibuni, Kocha Mkuu wa Simba, Goran Kopunovic alifunguka kuwa kuna kiongozi amekuwa akimpangia timu na kumuonyesha fomesheni ya kutumia.


Baadaye Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe akasema kocha alisema alikataa ushauri wa kiongozi huyo, hivyo haikuwa kulazimisha badala yake ni ushauri.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic