February 7, 2015


Kocha wa Simba, Goran Kopunovic, amempa masharti magumu beki wa timu yake hiyo, Joseph Owino ambaye amerejea uwanjani hivi karibuni baada ya kukaa nje ya uwanja kutokana na kusumbuliwa na majeraha ya nyama paja.


Owino alianza mazoezi mepesi wiki iliyopita na anatarajiwa kuanza mazoezi ya pamoja na wachezaji wenzake hivi karibuni, hivyo akirudi kikosini kutakuwa na vita kubwa ya namba kati yake na mabeki Hassan Isihaka na Juuko Murshid ambao kwa sasa wapo kwenye kiwango kizuri.

Kopunovic amesema hawezi kumpa nafasi kwa kuwa anahitaji kuangalia kiwango chake na nidhamu kabla ya kumpa nafasi ya kucheza licha ya kuwa Owino alikuwa nahodha wa timu hiyo kabla kocha huyo hajatua klabuni hapo.

“Owino ana nafasi ya kucheza japo mabeki wote wapo katika viwango vizuri, lakini siwezi kusema namhakikishia namba kwa sasa, lazima aonyeshe kiwango.

“Sipendi kumuona beki ambaye katika kila mchezo anapewa kadi au kusababisha penalti, kama hatakuwa na tabia hizo basi ana nafasi kubwa ya kucheza,” alisema Kopunovic.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic