February 7, 2015


Yanga, kesho Jumapili inatarajiwa kushuka uwanjani kukipiga dhidi ya Mtibwa Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, lakini kuna kitu cha kushangaza kimetokea.


Beki wa kati wa Mtibwa Sugar, Salum Mbonde ameibuka na kuipangia Yanga kikosi ambacho anaamini kinaweza kusaidia timu hiyo ya Jangwani kupata ushindi kwenye mchezo huo.

Mbonde ambaye pia aliibuka Mchezaji Bora wa Kombe la Mapinduzi 2015, amesema kuwa Yanga inatakiwa kutowachezesha Kpah Sherman na Amissi Tambwe katika mchezo huo.

“Tunakutana na Yanga kwa mara nyingine tena baada ya kuwafunga kwenye mechi ya kwanza, mimi nawapa ushauri tu kuwa, kama wanataka ushindi katika mchezo wetu huo, basi wanatakiwa kutowapanga akina Tambwe na Sherman, badala yake wawaanzishe Hussein Javu, Danny Mrwanda na wazawa wengine, vinginevyo itakula kwao.

“Wazawa wanajua jinsi ya kucheza mechi ngumu, hao Tambwe na Sherman siyo wachezaji wabaya lakini kutufunga sisi itakuwa ni ngumu,” alisema Mbonde.


Mtibwa iliifunga Yanga mabao 2-0 katika mechi ya kwanza ya msimu huu kwenye Uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic