February 18, 2015

Wachezaji na makocha wa Chelsea walilazimika ‘kupiga’ miguu umbali mdogo kutoka uwanjani baada ya basi lililokuwa linawapeleka uwanjani kukwama.


Basi hilo lilikwama katikati ya ukuta wakati likipita kuingia uwanjani kabla ya kuwashusha wachezaji ili waingie vyumbani kwenye Uwanja huo tayari kuivaa PSG.
 
Juhudi za dereva kulikwamua zilishindikana kwa zaidi ya dakika tano.
Kutokana na hali hiyo, Kocha Jose Mourinho aliamuru wachezaji na wengine waliokuwa ndani ya basi kushuka na kutembea hadi vyumbani.

Katika mechi hiyo jijini Paris, Chelsea waliokuwa wageni walipata sare ya bao 1-1. 





0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic