February 14, 2015


Na Saleh Ally
LIGI Kuu England imebakiza mechi 13 kwa kila timu itakuwa imefikia tamati huku Chelsea na Manchester City zikifukuzana kuwania taji la England.

Ukiwauliza mashabiki wengi katika mitaa mbalimbali ya majiji ya Dar es Salaam, Mwanza, Arusha, Mbeya na mikoa mingine watakuambia timu ambayo inaonekana kuyumba zaidi ni Manchester United.

Mvuto umepotea na inaonekana kutokuwa na lile soka la kukata na shoka. Lakini wengi hawaoni Man United inavyokwenda mwendo wa kimyakimya lakini ni wa kasi kubwa.

Man United bado wanaonekana ni hatari, hilo linathibitishwa na takwimu na si suala la hadithi au kuamini tu wamekwisha.

Hadi sasa wako katika nafasi ya tatu katika msimamo wakiwa na pointi 47, tofauti ya pointi tano tu na wapinzani wao Man City wenye pointi 52.

Kuna uwezekano mkubwa wa Man United ikawashangaza wengi kwa kumaliza ligi hata ikiwa katika nafasi ya pili. Kweli, hakuna ubishi ina upinzani mkubwa sana kutoka kwa Southampton yenye pointi 46 katika nafasi ya nne na Arsenal iliyo na alama 45 nafasi ya sita.

Kuanzia nafasi ya tatu hadi ya tano, mmoja akiteleza kidogo, mwingine anakwea. Lakini bado Man United ina nafasi ya kwenda nafasi ya pili hasa kama Man City itapoteza mechi moja na kutoka sare moja huku Man United ikishinda zote mbili.

Mwenendo wa Man United katika mechi tano zilizopita unaonyesha kuwa wa juu zaidi kuliko hata wa Man City, labda kama baada ya ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Stoke City itakuwa imeamka.


Katika mechi tano zilizopita, Man City imeshinda moja, sare tatu na kupoteza moja. Wakati Man United imeshinda tatu, sare moja na kupoteza moja.

Iwapo Man United itaweza kushikilia rekodi zake na kuendelea kufanya vizuri, itakuwa mtihani kwa Man City na kuna uwezekano mkubwa wa kupoteza nafasi hiyo ya pili kwa Mashetani hao wekundu wanaokwenda mwendo wa kimyakimya lakini wanasonga tu.

Kwa mwendo huo, utagundua kishabiki, Man United imekwama na haifanyi vizuri. Ila imepoteza yale yaliyozoeleka lakini bado haijaingia kwenye kundi la Liverpool na bado zikiwa zimebaki mechi 13, iko juu ya Arsenal ambayo bado inaonekana haifanyi vibaya sana.

Mazoea ya nafasi ndiyo tatizo hapa. Kwamba Arsenal kushika nafasi ya nne au tatu ndiyo kawaida, wakati United inajulikana kwa ubingwa na nafasi ya pili.

Ugumu zaidi kwa Man United ni zile mechi 13 zilizobaki, watalazimika kuzicheza kama karata kwa umakini mkubwa kwa kuwa wana mechi 6 tu nyumba na 7 zilizobaki ni ugenini.

Kwa msimu huu, ushindi mkubwa kwa Man United ni bao 4-0 dhidi ya QPR na kipigo kikubwa ni bao 5-3 dhidi ya Leicester. Lakini baada ya hapo inaonekana ni bora kwa kuwa imeweza kucheza mechi nane kabla ya kupoteza, pia imefanikiwa kushinda mara sita mfululizo.


Hii inaonyesha rekodi zake bado ziko juu kitakwimu, hivyo Man United bado ni timu isiyotabirika na inaweza kufanya lolote katika wakati ambao haukutarajiwa.

Iwapo Man United itacheza vema karata zake 13 zilizobaki angalau wakashinda mechi nane, basi wana nafasi kubwa ya kuwa katika nafasi ya pili au kubaki hiyo ya tatu na kuwapa kazi ngumu Arsenal, Southampton na Tottenham kugombea nafasi moja iliyobaki kukamilisha Top 4 kwa ajili ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Mechi:

Cheza 25

Bado 13

Zilizobaki:

Nyumbani 6

Ugenini 7



Ngumu:

Nyumbani: Vs Spurs, Man City, Arsenal

Ugenini: Vs Liverpool, Chelsea, Everton


MECHI 13 ZILIZOBAKI:

            Februari 21

Swansea V Man Utd

            Februari 28    

Man Utd V Sunderland    

            Machi 4

Newcastle V Man Utd

         Machi 15

Man Utd V Tottenham

         Machi 22

Liverpool V Man Utd

         Aprili 4

Man Utd V Aston Villa

    
        Aprili 11

Man Utd V Man City

        Aprili 18

Chelsea V Man Utd

         Aprili 25

Everton V Man Utd

        Mei 2

Man Utd V West Brom

      Mei 9

Crystal Palace V Man Utd

      Mei 16

Man Utd V Arsenal

      Mei 24

Hull V Man Utd





0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic