February 27, 2015

WACHEZAJI WA YANGA WAKIWA KATIKA UWANJA WA LOBATSE, BOTSWANA.

Yanga imeonyesha haitaki utani baada ya kumtimua Ofisa wa Jeshi la Botswana (BDF) mwenye cheo cha luteni ambaye alikuwa amefika katika Hoteli ya Oasis nje kidogo ya Jiji la Gaborone, Botswana.


Yanga wako jijini hapa kwa ajili ya mechi yao ya marudiano ya Kombe la Shirikisho dhidi ya BDF XI itakayopigwa leo kwenye Uwanja wa Lobatse.
 
MRISHO NGASSA NA SIMON MSUVA WAKILAMBA INTERVIEW YA CLOUDS TV WAKIWA KWENYE UWANJA WA LOBATSE NCHINI BOTSWANA AMBAKO LEO WANAKIPIGA HAPO.
Aliyeanzisha kasheshe hilo ni Katibu Mkuu wa Yanga, Dk Jonas Tiboroha ambaye alimtaka ofisa huyo wa jeshi kuondoka mara moja kambini hapo.

Hali hiyo ilionyesha kumuudhi sana ofisa huyo ambaye alilaumu kutokana na tukio hilo na kusisitiza kwamba katibu huyo hakuwa mwanamichezo, lakini Dk Tiboroha hakutaka kulizungumzia zaidi ya kusisitiza usalama wa kikosi chake ndiyo jambo muhimu.

“Ni kweli katibu amemtaka ofisa huyo aondoke katika eneo la hoteli. Unajua jana (juzi) walikuja hapa hotelini maofisa watatu, waliungana na sisi baada ya kuikataa Hoteli ya Grande,” alisema Mkuu wa Kitengo cha Habari cha Yanga, Jerry Muro na kuongeza:

“Sasa leo (jana) asubuhi amekuja mwingine mmoja ambaye alifika mapema hata kabla hatujaanza kunywa chai. Katibu akaona hilo siyo sawa, ukizingatia huyo ni mwanajeshi, akamfuata na kumueleza aondoke.

“Jamaa alichukia, ila nimekaa naye tena na kumuelezea kuwa hapa hotelini tunamhitaji mtu mmoja tu kutoka BDF. Sisi pia tulifanya hivyo na hakuna kiongozi wetu aliyekwenda kambini kwao walipokuwa Dar.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic