March 21, 2015


Rais wa Simba, Evans Aveva, ametoa maagizo mazito kwa benchi la ufundi la timu hiyo likiongozwa na Mserbia, Goran Kopunovic kuhakikisha wanashinda michezo yote iliyo mbele yao.


Mabingwa hao wa zamani wa Bara, wamebakiwa na michezo saba kabla ya kumaliza msimu huu ambayo ni sawa na dakika 630.

Simba ipo nafasi ya tatu ya msimamo wa ligi kuu kwa kuwa na pointi 29 nyuma ya Azam yenye pointi 33 na Yanga yenye 34.

 Aveva amesema kuwa moja ya mikakati waliyojiwekea ni kuhakikisha wanashinda michezo yote iliyobakia kwa kutoa maagizo katika benchi la ufundi kuhakikisha agizo hilo linatekelezeka.

“Kwa sasa hatutazami suala la ubingwa wa ligi msimu huu ila tunachotaka ni kuweza kushinda michezo yetu yote iliyobakia na tayari nimeshatoa maagizo katika benchi la ufundi kwa ajili ya utekelezaji.

“Tunahitaji kumaliza katika nafasi nzuri, hivyo ni lazima tufanye vyema katika mechi zilizobakia bila kupoteza,” alisema Aveva.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic