March 21, 2015


Maisha ya kiungo wa Simba, Shaban Kisiga ndani ya Msimbazi sasa unaweza kusema ndiyo yamefikia mwisho, kufuatia kauli tata iliyotolewa jana na uongozi wa klabu hiyo.


Kisiga hajawa na timu tangu Januari 28, mwaka huu baada ya kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Mbeya City huku kukiwa hakuna mawasiliano yoyote kati yake na waajiri wake.

Hata hivyo, Katibu wa Simba, Stephene Ally, amekata mzizi wa fitina baada ya kufunguka kwa kina kuhusu majaaliwa yake kwa kusema kuwa ni vigumu kurejea Simba kwa kuwa alishindwa kutekeleza masharti.

“Kisiga alijiondoa mwenyewe kikosini, tulifanya kila njia ya kuwasiliana naye na tukamwambia aandike barua kutueleza sababu iliyomuondoa kambini bila kuaga lakini amekataa kufanya hivyo.

“Sasa kama anasema anasubiria sisi kumpigia simu, tutaanzia wapi wakati yeye mwenyewe ameshindwa kutekeleza maagizo? Na tutaanzia wapi kumtafuta wakati utaratibu unajulikana!


“Cha msingi tunasubiria maamuzi yoyote yatakayofikiwa na kamati ya utendaji kuhusu suala lake na tutatangaza kama tulivyomtangaza rasmi,” alisema Ally.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic