March 30, 2015


Timu ya taifa ya soka la ufukweni ya Oman ndiyo mabingwa wa Asia na sasa watashiriki michuano ya Kombe la Dunia itakayofanyika nchini Ureno.


Kazi yote ni sifa zimuendee kocha wao mkuu, Talib Hilal ambaye ni beki wa zamani wa Simba.
TALIB AKITOA MAELEKEZO KWA KIKOSI CHAKE AMBACHO SASA NDIYO MABINGWA WA BARA LA ASIA NA WAWAKILISHI KATI YA WATATU WA BARA HILO KATIKA KOMBE LA DUNIA LITAKALOPIGWA NCHINI URENO.

Hilal ameipeleka timu hiyo fainali za Kombe la Dunia baada ya ushindi mfululizo  katika michuano ya Asia huku fainali wakiwatwanga Japap mabao 3-2 kwa mikwaju ya penalti.

Usisahau pamoja na Hilal, kocha msaidizi wa kikosi hicho ni Mtanzania, Yusuf Abeid, kipa wa zamani wa Pamba ya Mwanza.

Lakini kabla ya hapo walikuwa wamejihakikishia kucheza Kombe la Dunia baada ya kuwafunga Lebanon kwa mabao 5-4.

Kabla ya hapo, hatua ya robo fainali, Oman ya Talib walionyesha kweli wanajua baada ya kuwakung’uta China kwa mabao 7-2.


Michuano hiyo ya Asia iliunguruma jijini Doha, Qatar kuanzia Machi 23 hadi 28 na Oman ndiyo wababe zaidi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic