March 30, 2015

  

Louis van Gaal ameibuka mshinda wa tuzo maarufu ya Anton Geesink.


Tuzo hiyo maalum hutolewa nchini kwao Uholanzi kwa mtu, mji au kundi la watu lililofanya vema katika michezo.

Van Gaal ambaye amekuwa akihaha na kikosi chake cha Man United, amepewa tuzo hiyo baada ya Uholanzi kuonyesha kiwango bora na kushika nafasi ya tatu katika Kombe la Dunia nchini Brazil, mwaka jana.
 
Mambo yamekuwa si mazuri sana kwake akiwa na Man United, lakini sasa angalau iko katika nafasi ya nne katika msimamo wa Ligi Kuu England na wikiendi hii ina kibarua kigumu dhidi ya Aston Villa.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic