March 30, 2015


Timu ya Coastal Union ya Tanga, inaweza kuwa imeingia kwenye mtihani mzito baada ya kudaiwa kuwa kipa wake namba moja, Shabaan Kado, kagoma na kaondoka klabuni hapo kutokana na sababu mbalimbali.


Imeelezwa kuwa chanzo kikubwa cha yote hiyo ni kwamba kipa huyo hajafurahishwa na hali ya maisha yake ya sasa klabuni hapo ikiwemo kushutumiwa kwa baadhi ya mambo yanayoenda kombo klabuni hapo kwa sasa ikiwa ni pamoja na kutupwa benchi katika mechi mbili za mwisho za timu hiyo dhidi ya Ruvu Shooting na Azam FC na nafasi akapewa Fikirini Mapala.

Mtu wa karibu na Kado kutoka kikosini hapo alilijuza blogu hii kuhusiana na tukio hilo na kueleza ukweli kwamba Kado hajafurahishwa na vitendo hivyo, ndiyo maana ameamua kuondoka Tanga kwa siku ya tatu sasa na kurejea Dar es Salaam kwa ajili ya kutuliza akili.

“Huku mambo si shwari sana, Kado ameamua kuondoka hapa na amekwenda Dar kutuliza akili, anadai kwamba amechoshwa na baadhi ya maneno yanayoelekezwa juu yake kutokana na hali ya timu ilivyo sasa, mechi za Ruvu na Azam pia hakudaka na akajaribiwa kipa mwingine, hivyo hayo yote anaona bora ajitenge kwanza kwa sasa,” alisema mtoa taarifa huyo.

Alipotafutwa Kado mwenyewe kuzungumzia suala hilo, hakuweza kupatikana kutokana na simu yake ya mkononi kutokuwa hewani lakini Meneja wa Coastal, Akida Machai alisema:
 “Hapana, Kado hajaondoka kwa ubaya wowote hapa, alinitumia meseji kwenye simu yangu kwamba anaondoka kwenda Dar kumuangalia bibi yake anaumwa na kisha atarudi mapema kuja kuendelea na timu.”


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic