March 24, 2015

CRYUFF (KUSHOTO)...
Kocha wa zamani wa Barcelona na gwiji wa klabu hiyo, Johan Cruyff amesema hakufurahishwa na mchezo uwezo waliouonyesha Barcelona.


Cruyff raia wa Uholanzi ambaye alikuwa mchambuzi wakati wa mchezo huo, amesema hakufurahishwa na kiwango walichokionyesha Barcelona.


Hata hivyo alisisitiza, alifurahia ushindi wa mabao 2-1 kwa kuwa timu yake ndiyo iliyoibuka na ushindi.

“Si vibaya kufurahia ushindi wakati hamkuonyesha kiwango bora, lakini siwezi kusema ulikuwa ushindi bora,” alisema.


Barcelona ilifanikiwa kushinda kwa mabao 2-1 ikiwa nyumbani dhidi ya Real Madrid, hata hivyo haikuonyesha kiwango cha juu sana kama ilivyokuwa imetazamiwa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic