March 24, 2015


Yanga inashuka dimbani kesho kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam tayari kumenyana na JKT Ruvu ili kusaka pointi tatu muhimu.


Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van der Pluijm amesema pointi hizo tatu ni kuhimu kwa kuwa ndiyo watakuwa timu ya kwanza kufikisha pointi 40.
“Kushinda kila mechi ni muhimu, lakini mechi hii inaweza kuwa ni muhimu zaidi.

“Tukifikisha pointi arobaini litakuwa moja ya jambo muhimu katika kipindi hiki. Lazima tushinde na wachezaji wanalijua hilo.

“Tunajua hatuwezi kushinda kilahisi kwa kuwa ligi ni ngumu na kila timu ina kiwango bora,” alisema Pluijm.
Azam FC ndiyo inayoipa Yanga presha ya juu zaidi kwa kuwa ina pointi 36 ikiwa ni tofauti ya pointi moja tu.


Mabingwa hao watetezi nao wamekuwa na mwendo mzuri wa ushindi, hali inayoilazimu Yanga kuhakikisha haitelezi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic