March 25, 2015


MPIRA UMEKWISHA
Yanga wanaonekana kupoteza muda huku JKT angalau wakijitahidi kutafuta angalau bao la pili
DK 90+2
DK 90 Javu anajaribu shuti lake la kwanza baada ya kupokea pasi ya Nizar, hata hivyo mpira unapaa juuu

Dk 88 Nizar anaingia kuchukua nafasi ya Niyonzima aliyeumia

Dk 83 Haruna Shamte anapewa kadi ya njano kwa kumfanyia madhambi Ngassa.


Dk 80, Kamuntu anaruka mbele ya Twite na kupiga kichwa lakini kinakuwa hakina madhara. Wakati anainuka anafanya kitendo ambacho si cha kiungwana kwa kumpiga kiwigo.


Dk 75, Magulu anapiga shuti kali lakini Barthez anaonyesha ujuzi kwa kudaka kwa ufundi mkubwa.


Dk 74 Yanga wanamtoa Tellela anaingia Hassan Dilunga, wanamtoa Mrwanda anaingia Hussein Javu na JKT wanamuiniza Najib Maguku kuchukua nafasi ya Alex Abel. 

Dk 70, Niyonzima anapiga shuti safi lakini kipa Haule anaonyesha ujuzi kuokoa.
Dk 64, JKT wanaingia eneo la hatari lakini Makwaya anakuwa na haraka na mpira unaishia kwa Cannavaro anayeondoka hatari.

Dk 60, Ally Bilal anaingia kuchukua nafasi ya Amos Mgisa kwa upande wa JKT
Dk 59, Kamutu analambwa kadi ya njano kwa kumfanyia Ngassa rafu ya makusudi kabisa.


GOOOOOO Dk 56 Msuva anafunga bao la tatu baada ya Telela kugongeana na Ngassa aliyempa pasi safi mfungaji.


Dk 53 Damas Makwaya analambwa kadi ya njano kwa kujiangusha.Dk 51, kama kawaida, Msuva anapewa pasi nzuri na Mrwanda lakini anashindwa kufunga kwa kupaisha juu.


Kipindi cha pili kinaanza kwa kasi kila timu ikiwa imepania kushinda. Kidogo JKT wanaonekana kuchangamka.
MAPUMZIKO:

Dk 45, Samuel Kamuntu anaifungia JKT bao safi kwa shuti kali baada ya mabeki wa Yanga kuzubaa.

Dk 43 Yanga wanaonekana kumiliki mpira zaidi huku JKT wakitumia muda mwingi kukaba.


GOOOOOOOO Dk 41, Mrwanda anaifungia Yanga bao la pili baada ya kuwatoka mabeki wawili, akatoa pasi kwa Msuva ambaye anapiga krosi safi kwa mfungaji.

Dk 39, Mbaga naye anapata nafasi baada ya kuingia kwenye box, lakini anashindwa kutulia na kupiga shuti hovyooo

Dk 35, Msuva anapata krosi nzuri ya Juma Abdul, akiwa yeye na kipa hatua nne kutola langoni, anapiga kichwa lakini anashindwa kulenga.


GOOOOOOOO Dk 33 Msuva anafunga penalti hiyo vizuri kabisa na kumfikia mshambuliaji Didier Kavumbagu....


PENAAAAAT Dk 33 beki Makwaya anashika eneo la hatari na mwamuzi anaamuru penati ipigwe
Dk 29&32, JKT wanaonekana kubaki nyuma zaidi na hakuna mashambulizi yoyote wanayofanya huku wakibakiza mabeki wanne nyuma na kushambulia kwa kushitukiza lakini hawana shambulizi lolote kali.


Dk 28, Ngassa naye anapewa kupiga mpira wa faulo, vilevile naye anapaisha juuu
Dk 25, Joshua anapiga mkwaju wa faulo lakini anapaisha juuuu..
Dk 22, Ngassa anapoteza nafasi ya wazi akiwa yeye na kipa baada ya krosi nzuri ya Juma Abdul aliyekuwa amewatoka mabeki wa JKT.


Dk 20, Ngassa anawatoka mabeki wa JKT na kupiga shuti ambako linapanguliwa na kipa Benjamin Haule na mabeki wake wanaondosha hatari.

DAKIKA YA 1 hadi 15 Yanga ndiyo wanaonekana kujipanga zaidi kwa kufanya mashambulizi mengi.



Hata hivyo inaonekana wachezaji wa Yanga pia hawako makini sana katika umaliziaji. Bado mchezo pia haujachangamka kwa kiasi kikubwa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic