March 24, 2015



Yanga itaendelea kukosa huduma ya kiungo wake mwenye kasi Mrisho Ngassa.


Ngassa amefanya mazoezi leo asubuhi na kikosi hicho, lakini bado anaonekana kutokuwa fiti.

Hivyo ataukosa mchezo wa kesho dhidi ya Ruvu JKT kama alivyouokosa uliopita dhidi ya Mgambo Shooting mjini Tanga.
Ngassa aliuokosa mchezo huo kwenye Uwanja wa Mkwakwani huku Yanga ikishinda kwa mabao 2-0.

Hata hivyo, ilionekana wazi alikuwa akihitajika hasa kupitia kasi yake kubwa.


Ngassa amekuwa akilishirikiana na Simon Msuva kupandisha kasi ya mashambulizi ya Yanga na huenda akakaa nje kwa zaidi ya siku nyingine tatu zijazo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic