April 10, 2015


TALIB (WA PILI KUSHOTO) NA ABEID (ANAYEMFUATIA) WAKISHEREKEA BAADA YA KUTWAA UBINGWA WA GHUBA JIJINI DOHA, QATAR, JANA.
Oman imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ghuba kwa upande wa soka la ufukweni.


Oman inayofundishwa na beki wa zamani wa Simba, Talib Hila na kipa wa zamani wa Pamba, Yusuf Abeid imeshinda mechi zake zote tano.
 
TALIB AKITOA MAELEKEZO...
Oman ambao kwa sasa ndiyo mabingwa wa dunia walianza kwa kuwachapa Bahrain kwa mabao 4-3, halafu wakawapa kipigo wenyeji Qatar 4-1.
Kama hiyo haitoshi wakawachapa Kuwaiti kwa mabao 4-2 kabla ya kuishushia kipigo UAE cha mabao 5-3.

Hivi karibuni Talib na mwenzake Abeid, waliingoza Oman kubeba ubingwa wa dunia pia kupata nafasi ya kushiriki Kombe la Dunia litakalofanyika nchini Ureno.


Timu ya taifa ya Oman ya soka la ufukweni inaonekana kuwa tishio kwa upande wa bara la Asia.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic