April 10, 2015

WACHEZAJI WA ETOILE DU SAHEL WAKIJIFUA VILIVYO KABLA YA MECHI KADHAA ZA LIGI KUU YA TUNISIA PAMOJA MECHI YA KOMBE LA SHIRIKISHO DHIDI YA YANGA.
 Yanga imepita kwa kishindo kutoka hatua ya awali, ya kwanza na sasa imetinga hatua ya pili ya Kombe la Shirikisho.


Imevuka kwa kuzifunga timu za BDF ya Botswana na baadaye FC Platnum ya Zimbabwe.

Hauwezi ukasema Yanga ilizitoa timu nyanya sana kwa kuwa tuliona namna zilivyocheza. Huenda kikosi cha Yanga kilikuwa katika ubora sahihi.
 
Bado Yanga haijafika katika safari iliyokuwa inahitaji kufika, vita iko mbele na inabidi kupambana zaidi ya ilipo.

Sasa inakutana na Etoile du Sahel ya Tunisia, timu ambayo ina kumbukumbu ya kung’olewa na Simba katika michuano ya kimataifa.

Lazima inajua machungu au ugumu wa timu za Tanzania na inajua kuwa Yanga ni moja ya klabu kongwe barani Afrika.

Kamwe haiwezi kufanya utani, ndiyo maana ukifuatilia, wameanza mazoezi mapema, wanapambana vilivyo na wamepania kushinda.

Yanga hawapaswi kulala kwa kufurahishwa na matokeo ya mechi zao nne za Kombe la Shirikisho dhidi ya BDF XI na FC Platnum.
 
Lakini bado hawatakiwi kusinzia na kuridhishwa na matokeo yao dhidi ya timu za Tanzania Bara ambako imefikia hadi kuzikaanga timu kongwe kama Coastal Union kwa mabao 8-0.

Kikosi cha Yanga kina mwelekeo mzuri wa kuwa imara, lakini bado hakijasimama katika hali ya kuwa tishio sana hadi kwa timu kama Etoile.

Lakini ilipofikia pia, haiwezi kuwa timu dhaifu ya kuihofia Etoile hadi watu wachanganyikiwe. Kikubwa ni umakini, malengo na viongozi watambue wanakutana na timu ya namna gani na nini cha kufanya.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic