April 27, 2015



Kiungo nyota wa Chelsea, Eden Hazard ametangazwa kuwa mchezaji bora wa Ligi kuu England kwa wachezaji wote wa kulipwa.


Hazard ameshinda tuzo hiyo ya PFA kwa mwaka 2015.
Raia huyo wa Ubelgiji mwenye miaka 24 tayari ameisaidia Chelsea kutwaa ubingwa wa Capital One na yuko njiani kuisaidia kubeba ubingwa wa Ligi Kuu England.



Tayari ameshafunga mabao 18 akiwa na Chelsea msimu huu na anazidi kuonekana ni mchezaji tegemeo zaidi huku Chelsea ikiutaka ubingwa huo kwa udi na uvumba. Mara ya mwisho iliubeba mwaka 2010.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic