April 27, 2015


Kocha wa Coastal Union, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ ambaye hajawahi kuipenda Yanga hata kwa utani, ameibuka na kuipa timu hiyo mbinu za kuiua Etoile du Sahel ya Tunisia katika mchezo wa Kombe la Shirikisho.


Julio alisisitiza kuwa, ili waweze kufanikiwa kuwaondoa Waarabu hao, wanatakiwa kwenda kwa tahadhari na kuepuka fitna zao.

Yanga inatarajia kurudiana na Etoile kati ya Mei Mosi hadi tatu nchini Tunisia, baada ya mchezo ule wa awali kutoka sare ya bao 1-1 Uwanja wa Taifa jijini Dar, hivyo inalazimika kupata sare ya zaidi ya bao moja au ushindi ili kusonga mbele.

Julio amesema kuwa Yanga ina kibarua kigumu cha kuhakikisha inafanikiwa kuwaondoa wapinzani wao katika michuano hiyo na kudai kuwa Waarabu wana fitna sana, hasa wanapokuwa nyumbani kwao.

“Yanga wanatakiwa kwenda kucheza kwa tahadhari kubwa ili waweze kushinda katika mchezo wa marudiano kwa kuwa Waarabu ni watu wenye fitna sana.

“Mchezo wa marudiano utakuwa mgumu, hivyo wanahitaji kujipanga na kutathmini mchezo uliopita na kuhakikisha wanafanya vyema katika mchezo unaofuata, naamini hakuna kitakachoshindikana iwapo kutakuwa na mipango madhubuti,” alisema Julio.




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic