April 12, 2015



Kamati ya Rufaa ya Nidhamu (TFF) imekutana leo tarehe 12/04/2015 kujadili rufaa No. 1/2014 ya DR DAMAS  NDUMBARO dhidi ya TFF.


TFF iliwakilishwa na Wakili Msomi Emmanuel Muga na Dr. Ndumbaro hakufika wala hakuwakilishwa na wakili wake.

Kufuatia kutofika kwa Dk Ndumbaro, Kamati, kwa Azimio moja, iliamuru TFF itoe wito mpya na  mpaka tarehe 14/04/2015 uwe umemfikia Dr. Ndumbaro, ukimfahamisha tarehe ya kikao kijacho cha kusikiliza rufaa yake.

Lakini taarifa za uhakika za awali ziliyoifikia SALEHJEMBE kupitia mmoja wa wajumbe wa kamati ya rufaa ya TFF zilionyesha Dk Ndumbaro hakuwa ameelezwa lolote.

Pia kama ilivyo kawaida ya TFF imekuwa ikitoa taarifa kwa waandishi siku ya kusikilizwa kwa rufaa mbalimbali, haikufanyika hivyo.

Rufaa hiyo ya Dk Ndumbaro kupinga kufungiwa miaka mitano ilipangwa isikilizwe kwa siri.

Lakini leo, imeshindikana baada ya baadhi ya waandishi kuanza kupiga simu wakihoji kuhusiana na rufaa hiyo huku wakitaka kujua kama Dk Ndumbaro ambaye ni mlalamikaji ana taarifa.

“Tumeona tutaaibika, maana kila mtu ameanza kuuliza. Hii ya kutaka kusikiliza bila ya kumtaarifu mlalamikaji tumeona itatufanya tuonekane ni watu wa kubahatisha.

“Tumewataka TFF wampe taarifa ili awepo, hata kama mnamuuma mtu basi lazima muonyeshe kufuata utaratibu ndigu yangu aaah!” kilieleza chanzo cha uhakika kutoka ndani ya kamati hiyo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic