April 11, 2015

Mechi ya kesho ya Ligi Kuu England kati ya watani na wapinzani wakubwa Manchester United dhidi ya Manchester City inaaminika ndiyo ghali zaidi.


Mechi hiyo itapigwa kwenye Uwanja wa Old Trafford inaaminika ndiyo ghali zaidi katika mji huo, lakini ghali zaidi katika soka la England.

Timu hizo zinakutana wakati Man United imetumia kitita cha pauni milioni 278.2 kwa ajili ya usajili wakati Man City ndani ya misimu mitatu wamemwaga pauni milioni 244.7.

Lakini kwa hali ilivyo, bado inaonekana timu zote hazina uhakika sana wa kutwaa ubingwa.
Iwapo Man United itamfunga City, basi itakuwa imemuondoa kwenye mbio za ubingwa wa asilimia 80.

Ushindi kwa Man United pia utakuwa muhimu kwa kuwa itahitaji kupata moja ya nafasi kati ya nne za juu ili kushiriki Ligi ya Mabingwa.

Man Unite iko katika nafasi ya tatu ikiwa na pointi  62 na City ya nne ikiwa na 61.

Memechi ya kesho itakuwa ni ya 32 wa kila timu na kila moja itabakiza mechi sita kupigania ubingwa au kupata nafasi nne za juu.


United imekuwa ikibadilika na kurejea katika kasi yake huku City ikiporomoka kutoka katika ubora iliokuwa nao hadi kuonekana inabahatisha kiana.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic