April 20, 2015


Licha ya Yanga kuanza kwa sare ya 1-1 nyumbani katika mchezo wao wa awali wa raundi ya tatu dhidi ya Etoile du Sahel ya Tunisia, wachezaji wa kutumainiwa Yanga, Mrisho Ngassa na Simon Msuva, wametamba kuwa katika mechi ya marudiano watafanya maajabu na kuwatoa wapinzani wao.


Mchezo huo wa kuwania kufuzu kuingia kwenye hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho ulipigwa juzi Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa na unatarajiwa kurudiwa nchini Tunisia baada ya wiki mbili zijazo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo, wachezaji hao walisema kwamba wapinzani wao ni wazuri lakini si wa kuwapa nafasi kubwa katika mechi yao ya pili kwa kuwa kiuwezo ni watu wanaolingana isipokuwa kilichotokea siku hiyo ni makosa madogo ndiyo yaliwaponza.

“Ni wazuri lakini si kwamba walituzidi sana, isipokuwa ni makosa ya kimpira madogomadogo ya uwanjani ndiyo yalisababisha sare, kwa hatua hiyo hatuwezi kusema kwamba tumetoka, hatuwezi kukata tamaa, huu ni mpira na lolote linaweza kutokea hata huko kwao, tutakwenda Tunisia kupambana na tutafanya maajabu,” alisema Ngassa.

Kwa upande wa Msuva, alisema: “Jamaa siyo wabaya, kiuwezo ni wa kawaida, hauwezi kusema kama kwa matokeo haya, ndiyo tumetoka, bado tunataka kusonga mbele na morali hiyo tunayo, tutakwenda kwao kucheza mpira na kuhakikisha tunavuka hapa tulipo.”

Matokeo ya sare ya 1-1, yanaiweka Yanga katika mazingira magumu katika mechi ya pili huku ikitazamiwa kama watapata suluhu watakuwa wametoka, wakitoka 1-1 tena, hatua ya matuta itaamua na kama ikiwa ni sare ya 2-2 na kuendelea basi itakuwa neema kwa Yanga.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic