April 22, 2015


Katika kuhakikisha wanakuwa fiti kwa ajili ya mechi ya leo dhidi ya Mgambo JKT, kiungo mshambuliaji wa Simba, Mganda, Emmanuel Okiwi na beki wa pembeni, Hassani Kessy, wametengwa na kupewa mazoezi maalum.


Simba inatarajiwa kuvaana na Mgambo leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, katika mechi ya Ligi Kuu Bara.

Hiyo yote ni katika kuwaweka fiti wachezaji hao tegemeo wenye kasi baada ya kuikosa mechi iliyopita dhidi ya Mbeya City kwa matatizo tofauti, mchezo ambao ulimalizika kwa Simba kufungwa mabao 2-0.

Okwi aliikosa mechi ya Mbeya City kutokana na adhabu ya kadi tatu za njano huku Kessy yeye akiwa na matatizo na uongozi baada ya kugomea mazoezi ya timu hiyo akidai kumaliziwa fedha yake ya usajili na nyumba ya kulala.

Wachezaji hao, wakiwa chini ya kocha msaidizi, Selemani Matola, walipewa mazoezi ya kukimbia mbio fupi na ndefu kwenye Uwanja wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam baada ya kocha mkuu wa timu hiyo, Mserbia, Goran Kopunovic kupendekeza.

Wachezaji hao, walitumia kama dakika 15 kufanya programu hiyo maalum kuanzia saa 10:30 hadi 11:15 kabla ya kutakiwa kunywa maji na kupumzika.


Chanzo makini kutoka ndani ya Simba kimesema kuwa kocha huyo anafanya hivyo ili kuhakikisha wachezaji hao wanacheza leo kwa kuwa ni mechi muhimu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic