April 22, 2015


Katika kuhakikisha kikosi cha Coastal Union kinakuwa bora na cha ushindani msimu ujao, kamati ya usajili wa timu hiyo imejipanga kusajili wachezaji wenye uwezo kulingana na mahitaji huku wachezaji wote wa kigeni wakifunguliwa milango ya kuondoka kutokana na wote kumaliza mikataba yao.


Coastal ina wachezaji wanne wa kigeni ambao ni mshambuliaji Rama Salim (Kenya), Ike Bright Obina (Nigeria), Lutimba Yayo (Uganda) na Itubu Imbem (DR Congo) ambao wote mikataba yao inamalizika mwishoni mwa msimu.

Kiongozi wa kamati ya usajili wa timu hiyo, Salim Bawazir, amesema msimu ujao watakuwa makini kwenye suala ya usajili.

“Wachezaji wengi wanamaliza mikataba yao lakini kwa upande wa maprofesheno, nao wote wanamaliza mikataba, ambaye atakuwa tayari kubaki hakuna shida lakini ni ruksa hata kuondoka.


“Malengo yetu ni kuwabakiza wachezaji wengi wenye msaada kwenye timu,” alisema Bawazir.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic