April 1, 2015


Katika kuhakikisha wanakuwa na kikosi bora zaidi msimu ujao, Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van der Pluijm, amependekeza wasajiliwe wachezaji wanne kwa ajili ya kuongeza nguvu kwenye kikosi chake.


Yanga imekuwa ikimtumia Amissi Tambwe kama mshambuliaji wa kati ambapo hana msaidizi hadi sasa iwapo atapata majeraha kutokana na Kpah Sherman kutokuwa fiti.

Chanzo kutoka ndani ya Yanga kimeeleza wapo katika mikakati ya kusaka wachezaji wanne kwa ajili ya usajili wa msimu ujao ili kuimarisha kikosi hicho kwa ajili ya ligi na michuano ya kimataifa.

Nafasi ambazo zinatarajiwa kuzibwa katika usajili wa msimu ujao ni pamoja na walinzi wa pembeni, kiungo, washambuliaji wa kati na viungo wa pembeni ili kuweza kuimarisha kikosi.

“Tunahitaji kukiboresha zaidi kikosi msimu ujao kwani kumekuwa na upungufu mkubwa katika safu ya ushambuliaji, jambo ambalo uongozi umekutana na kocha ambaye ametaka nafasi hizo zifanyiwe kazi.

“Mchakato bado unaendelea na tumepanga kuongeza wachezaji katika nafasi nne ambapo suala la ushambuliaji ndilo limekuwa tatizo zaidi.

“Kwa sasa tunatafuta viungo wa pembeni pamoja na wa kati ili kuja kusaidiana na Tambwe, tunaamini tukileta mchezaji mwenye uwezo mzuri Tambwe atakuwa huru zaidi.


“Nafasi nyingine ni pamoja na walinzi wa pembeni na viungo ambao tunaamini wataimarisha timu, kwa sasa bado tunaendelea kuangalia wachezaji kutoka timu mbalimbali za ligi kuu,” kilisema chanzo hicho.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic