April 2, 2015


Mshambuliaji tegemeo wa Yanga, Amissi Tambwe amesema Yanga ia nafasi ya kushinda mechi yake ya ugenini ya Kombe la Shirikisho dhidi ya FC Platinum.


Yanga inaondoka nchini kesho kwenda Zimbabwe kuwafuata FC Plutnum katika mechi ya pili baada ya kuwa imeshinda kwa mabao 5-1 katika mechi ya kwanza jijini Dar.

“Mechi itakuwa ngumu kama hapa nyumbani, kwani katika soka wakati mwingine nyumbani na ugenini hakuna tofauti.

“Kikubwa ni sisi kujituma na kufanya vizuri, kocha anajua tunahitaji nini na sisi tunajua tumeelekezwa nini,” alisema tambwe.

“Tuna kikosi kizuri, ninawaamini wenzangu na kama tukitulia, naamini tunaweza kushinda hata ugenini.”


Tambwe ni kati ya waliofunga katika ushindi huo dhidi ya Platinums jijini Dar.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic