April 20, 2015

YANGA WAKISHANGILIA BAO BAADA YA NAHODHA CANNAVARO KUFUNGA BAO...

Ligi Kuu Bara inatarajia kuendelea kesho kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam wakati vinara wa ligi hiyo Yanga watawakaribisha timu ya Stand United kutoka mjini Shinyanga.


Yanga inaonekana kuwa na hasira baada ya kupata sare katika mechi yao ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Etoile du Sahel.

Kesho itakuwa na kazi kubwa ya kurudisha imani ya mashabiki wake na lazima ionyeshe kiwango ili kuamsha matumaini kwamba itafanya vema katika mechi ijayo dhidi ya Waarabu huko nchini Tunisia.

Stand nao wametamba kwamba hawako nalenale na wanataka kupambana na kushinda mechi hiyo kuwa na uhakika zaidi wa kubaki Ligi Kuu Bara.


Si lahisi kwa kila upande lakini Yanga lazima ishinde ili kujiweka sawa kwa kuwa tofauti ya pointi kati yake na Azam FC ni nne tu na Yanga ina mchezo mmoja mkononi kwa kuwa Aam FC imeshuka dimbani mara 22 na yenyewe 21.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic