April 8, 2015


Baada ya kumalizika kwa michuano ya ligi ya mkoa wa Dar es salaam na kupata timu tatu zitakazouwakilisha mkoa katika michuano ya ligi ya mabingwa ya mikoa ya TFF sasa ni fainali ya bingwa wa jumla kwenye Uwanja wa Karume jijini, kesho.


Timu zinazokutana kesho katika fainali hiyo ni Zakhem FC dhidi ya FFU SC ambazo zitashuka dimbani majira ya Saa 10 Jioni.

Kwa mujibu wa kamati ya mashindano ya Chama cha Soka Dar es Salaam (DRFA), timu zilizofanikiwa kuuwakilisha mkoa katika michuano ya ligi ya maabingwa ni pamoja na Zakhem FC, FFU SC na Changanyikeni SC.

Mwenyekiti wa DRFA, Almas Kasongo,ameipongeza kamati hiyo ya mashindano kwa kusimamia vizuri uendeshaji wa ligi tangu ilipoanza.

IMETOLEWA NA MSEMAJI WA DRFA, OMARY KATANGA.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic