May 8, 2015


Mwaka wa neema Jangwani! Wakati wakiwa kwenye shangwe za ubingwa, wachezaji wa Yanga wamezidi kupata ‘madili’ nje ya nchi, ambapo Simon Msuva, Mrisho Ngassa wanahitajika Afrika Kusini huku straika Dan Mrwanda akipata ofa nchini Thailand.


Mtu wa karibu na nyota huyo amesema kuwa, Mrwanda anataka kuwaandikia barua Yanga akitaka aachwe punde tu baada ya ligi kumalizika ili awahi dirisha la usajili nchini humo.

Chanzo hicho kimesema iwapo viongozi watamgomea kutokana na kuwa na mkataba, atakubali yaishe lakini ndoto yake ni kusaka changamoto kwingine. Alisaini mwaka mmoja akitokea Polisi Moro.

“Kuna timu moja nchini Thailand inamtaka na anasema ni lazima aende, lakini yote itatokana na baraka za viongozi wa Yanga. Baada ya ligi amepanga kuwaandikia barua ya kuomba aachwe ili awahi usajili ambao kwao unapishana na Tanzania,” alisema rafiki huyo.


Alipoulizwa Mrwanda, alisema: “Ni mapema sana, tungoje ligi iishe mengine yatafuata baadaye.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic