May 8, 2015


Beki kiraka wa Yanga, Mbuyu Twite, yupo nje ya kikosi cha Yanga kutokana na kusumbuliwa na malaria lakini ameweka mipango yake ya kusafiri akipitia Kenya kuzungumza na Gor Mahia juu ya masuala ya usajili kisha kwenda kwa Waarabu wa El Merreikh.


Twite ameliambia gazeti hili kuwa, akitokea Kenya ataenda DR Congo kumuona mama yake anayesumbuliwa na ugonjwa wa moyo kisha ataonana na viongozi wa El Merreikh ya Sudan.

“Malaria inanisumbua ndiyo maana nipo nje ya uwanja lakini nitaondoka muda wowote ndani ya siku mbili hizi kwenda nyumbani kumuona mama nikipitia Kenya.

“Nahitaji kuzungumza na viongozi wa Gor Mahia, walishanipigia simu tukaelewana, nikifika huko tutazungumza zaidi,” alisema Twite na kuongeza:


“Nikimalizana na Gor Mahia nitakutana na Merreikh nikiwa Congo, nilizungumza nao kuwa nikienda Congo tutakutana tuzungumze.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic