May 8, 2015


Baada ya kikosi cha Simba kushindwa kupata tiketi ya kushiriki michuano ya kimataifa kwa msimu wa tatu mfululizo, kocha na mchezaji wa zamani wa timu hiyo, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ amesema ni aibu kwa klabu kubwa kushindwa kushiriki kimataifa.


Julio amesema kuwa viongozi na wachezaji wameshindwa kuitendea haki klabu hiyo na badala yake wanaangalia zaidi maslahi binafsi.

“Hawaitendei haki Simba ile ambayo mimi naifahamu tangu enzi hizo, hii ni kutokana na aina ya viongozi waliopo pamoja na wachezaji kuendekeza starehe.

“Kitu kingine ni kubadili makocha kila kukicha, hicho nacho kimesababisha wapoteze mwelekeo. Wanatakiwa kujipanga upya wasajili wachezaji wenye uwezo,” alisema Julio.


Simba inashika nafasi ya tatu katika Ligi Kuu Bara na haitaweza kushiriki kimataifa, nafasi ambayo imetua kwa Yanga na Azam.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic