May 1, 2015


Kocha wa zamani wa Yanga, Marcio Maximo na aliyekuwa msaidizi wake klabuni hapo, Leonardo Neiva, wamefurahishwa na timu yao hiyo kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara hata kabla ya msimu kumalizika.


Makocha hao ambao ndiyo waliokuwa wakiifundisha timu hiyo mwanzoni mwa msimu huu, wametuma salamu za pongezi kwa viongozi, wachezaji na mashabiki wa klabu hiyo.


Akizungumza kutoka Brazil, Neiva ambaye kwa sasa anainoa timu ya Prudentopolis ya Brazil, alisema yeye na Maximo wamezipokea taarifa hizo kwa furaha na kwa pamoja wanaipongeza Yanga kwa hatua hiyo.

“Nimefurahi kusikia Yanga ndiyo mabingwa wa ligi, sikuweza kuficha furaha yangu, Maximo naye amezipata taarifa hizo, amefurahi pia.


“Kwa pamoja tunawapongeza wachezaji waliopambana hadi kufikia hapo bila kuwasahau viongozi na wote waliofanikisha hilo,” alisema Neiva ambaye yeye na Maximo walifukuzwa Desemba, mwaka jana baada ya kufungwa na Simba katika mechi ya Nani Mtani Jembe.

SOURCE: CHAMPIONI

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic