May 1, 2015

Kocha wa Yanga, Hans van der Pluijm amesema bado wana matumaini ya kupambana na kufanya vema dhidi ya Etoile du Sahel.

Pluijm ambaye yuko mjini Sousse, Tunisia na kikosi cha Yanga kwa ajili ya kuivaa Etoile du Sahel amesema matumaini ni makubwa lakini lazima wapambane.
“Tunajua tokea mwanzo haitakuwa kazi lahisi, lakini tuna matumaini ya kufanya vema. Ila lazima tupambane kweli kwa kuwa wana kikosi kizuri,” alisema.

Wachezaji wa Yanga wameonekana kuwa na morali na wako tayari kwa ajili ya mechi hiyo.

Leo asubuhi wachezaji hao pamoja na benchi la ufundi na viongozi, wamepata kifungua kinywa pamoja.






1 COMMENTS:

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic