May 7, 2015

MSUVA AKIWA KWENYE UWANJA WA SOCCER CITY JIJINI JOHANNESBURG, JANA.

Kiungo Simon Msuva anatarajia kuanza majaribio katika kikosi cha Bidvest Wits leo.


Timu hiyo maarufu kwa mashabiki kama Wits inashika nafasi ya nne katika Ligi Kuu ya Afrika Kusini.

Mmoja wa marafiki wa Msuva aliyeko jijini Johannesburg amesema kiungo huyo atafanya majaribio kwa siku tatu.

“Wamesema hadi Jumamosi, baada ya hapo ataanza safari ya kurejea Tanzania.

“Yuko hapa, amefika salama na tulikuwa naye uwanjani wakati Wits ikishinda kwa mabao 2-1 dhidi ya wakongwe Kaizer Chiefs jana,” alisema.

Timu hiyo inamilikiwa na Chuo Kikuu kikongwe barani Afrika cha Bidvest kilicho katikati ya jijini la Johannesburg.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic