Na Saleh Ally
BODI ya Ligi imetumia wataalamu wake kudadavua
mambo kadhaa hadi kufikia kuwatangaza wachezaji na makocha bora wa msimu
uliopita wa Ligi Kuu Bara.
Moja ya mambo ambayo yaliwashangaza wengi
lilikuwa ni lile la Kocha Mbwana Makata wa Prisons kuwa Kocha Bora wa Msimu wa
2014-15.
Makata ametangazwa kuwa kocha bora wa msimu
baada ya kushiriki mechi tisa tu. Kati ya hizo amefanikiwa kushinda nne, sare
nne na kupoteza moja.
Katika mechi tisa, Makata alikusanya pointi 16
na kuisaidia Prisons kuepuka kuporomoka daraja na kuiwezesha Mbeya kubaki na
timu mbili katika Ligi Kuu Bara.
Makata amekuwa kocha bora baada ya kuwashinda
makocha wawili wageni, Goran Kopunovic wa Simba aliyeiwezesha timu yake kushika
nafasi ya tatu na Hans van Der Pluijm aliyeipa Yanga ubingwa.
Ukiiangalia rekodi ya Makata ya mechi tisa na
kukusanya pointi 16, akiwa ameshinda mechi tatu na sare mbili nyumbani,
amepoteza moja, sare moja na kushinda moja akiwa ugenini, bado haitoshi kumpa
nafasi ya kuwa kocha bora.
| MALINZI NATIMU YAKE YA TFF; WASIIACHIE BODI YA LIGI IFANYE INAVYOTAKA. |
Kaiokoa timu kuteremka daraja, sawa. Lakini
kuna kocha aliyeipa timu ubingwa, kuna kocha aliyeipa timu nafasi ya tatu na
zote zilikuwa katika hali mbaya.
Kopunovic aliichukua Simba ikiwa taabani
kutoka kwa Phiri, akaibadilisha, ikaanza kuonyesha soka la kuvutia na kihesabu
inaonekana ndiyo timu iliyofanya vizuri zaidi katika mzunguko wa pili kuliko
nyingine zote.
Simba ni kati ya timu zilizofungwa mabao
machache zaidi na tuliona hata soka lake lilikuwa ni la kuvutia. Hivyo kocha
anayeonekana kuwa na ubora kati ya Makata na Mserbia huyo, jibu liko wazi
kabisa.
Ukirudi kwa Pluijm, unakumbuka wakati
anaichukua timu kutoka kwa Marcio Maximo. Ilionekana iko taabani, uchezaji wake
wa kubahatisha, lakini kafanya mabadiliko makubwa.
Mwisho Yanga imekuwa ni ya uhakika na tishio,
imemaliza msimu ikiwa timu iliyofunga mabao mengi zaidi, iliyofungwa machache
zaidi na ndiyo mabingwa.
Sasa kocha aliyeisaidia timu kutoshuka daraja
inawezekana vipi akawa bora kuliko huyo? Ukiangalia wastani wa ushindi, sare na
kupoteza kati ya makocha hao watatu, ule wa Makata unaonekana uko chini.
Mechi tisa kapoteza moja. Nane zilizobaki
kazigawa kwa sare na ushindi. Ushindi wa zaidi ya mechi kumi kutoka kwa Pluijm,
vipi awe chini ya Makata?
Ukiangalia unaona kuwa uteuzi umefanyika kwa
kuangalia mambo mawili. Moja inawezekana ni imani ya uzalendo au kutaka
‘kubalansi’ mambo na fulani apate.
Kwamba huyu ni mzalendo mwenzetu, kwa nini
tuwape Wazungu tu? Au tuzo zote watachukua na Simba pekee, basi tuangalie na
timu nyingine ili ‘kubalansi’ na kuwapa nguvu, kosa kubwa.
Iko haja ya kumuacha kila mmoja asimame kwa
miguu yake. Kuwapa wazalendo tuzo wasizostahili, ni kuwadanganya na kuzidi
kuwadumaza.
Pili ni suala ambalo nimelisikia. Kwamba
hakukuwa na watu imara kwa maana ya utaalamu waliofanya kazi hiyo ya uteuzi.
Lakini kati ya wajumbe, baadhi walikuwa na mchezo mchafu wa kuzigeuza tuzo hizo
kuwa mradi wa kujifaidisha kwa kuwa wadhamini walikuwa wanatoa zawadi za fedha.
Kuna mchezaji mmoja amelalamika kwamba kwa
kuwa yuko katika kundi la wale wanaogombea, basi alipigiwa simu na kuambiwa
afanyiwe mpango wa kushinda moja ya kipengele halafu fedha atagawana na mhusika
na wenzake.
Nimeambiwa kazi ya uteuzi wa wajumbe na
upatikanaji wa washindi ilifanywa na watu wa Bodi ya Ligi. Huenda wapo
waliokuwa na nia nzuri, lakini kuteua kwa kutozingatia vigezo kumekuwa tatizo
kwa kuwa wapo wanaotaka kujifaidisha wao, matumbo yao na familia zao na si
mpira wa Tanzania.
Hivyo wanaona, mchezaji anayekubali kugawana
zawadi yake, ndiyo anakuwa na nafasi ya kupata ushindi bila ya kuangalia kama
ni sahihi au la.
Sitaki kwenda mbali kuhusiana na ushindi wa
wengine. Huu wa Makata kwangu ulikuwa ni mfano tosha kwamba kuna madudu ndani
ya kazi hii ya utoaji tuzo.
Kama itaendelea, mwisho itapoteza maana na
wenyeji au wazalendo watakuwa wakidanganyika kwa ubora usio sahihi.
Wale wanaotaka kuzigeuza tuzo hizo kama mtaji
au mradi, wanapaswa kubadilika na kujua wanachafua mbio za maendeleo ya mpira
wa Tanzania.
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), lina dhamana
kubwa katika suala la heshima ya Tanzania. Hata kama Bodi ya Ligi Tanzania
ndiyo wahusika. Basi kuna wakati linapaswa kusimamia ubora wa mambo yanayoweza
kuvuruga heshima ya soka Tanzania. Hili ni mfano na Jamal Malinzi na timu yake
wafungue macho.
MBWANA MAKATA AMEIONGOZA PRISONS MECHI
9
SHINDA 4
SARE 4
POTEZA 1
Machi 14, 2015
Prisons
3-0
Stand
Sokoine
Laurian Mpalile 30
Salum Kimenya 65
Hamis Maigo
Machi 22, 2015
Prisons
0-0
Polisi
Moro
Sokoine
Aprili 4, 2015
Coastal
0-1
Prisons
Mkwakwani
Jeremiah Juma 44
Aprili 11, 2015
Ndanda
0-0
Prisons
Nangwanda
Aprili 15, 2015
Mtibwa
1-0
Prisons
Jamhuri
Aprili 19, 2015
Prisons
1-1
Mtibwa
Sokoine
Lugano Mwangama 77
Mgosi 40
Aprili 26, 2015
Prisons
2-0
Mgambo Sokoine
Fred Chudu 16
Boniface Hau 87
Mei 2, 2015
Prisons
1-0
Mbeya
Sokoine
Lugano Mwangama 90 (penalti)
Mei 9, 2015
Kagera
0-0
Prisons
Kaitaba
Fin.







0 COMMENTS:
Post a Comment