June 15, 2015

ABOAGYE AKIPAMBANA NA OKWI KATIKA MAZOEZI YA SIMBA

Mshambuliaji Aboagye Geirson raia wa Ghana aliyekuja kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa Simba, amepata dili la kwenda kukipiga nchini Thailand.

Mghana huyo, hivi karibuni alitua kufanya majaribio Simba lakini alishindwa kufuzu wakati mazoezi ya timu hiyo yakiwa yanasimamiwa na Mserbia, Goran Kopunovic.

Geirson alifanya majaribio hayo kwa muda wa wiki moja kwenye Uwanja wa Chuo Kikuu jijini Dar es Salaam lakini akapigwa chini.

Meneja wa mchezaji huyo, Gibby Kalule, alisema mshambuliaji huyo ametimkia Thailand Ijumaa iliyopita akitokea Nairobi, Kenya alipokwenda kuchukua viza.

Gibby alisema, amekwenda nchini humo kwa ajili ya majaribio baada ya kupata ofa kwenye klabu moja ambayo ni mapema kuitaja kwa hivi sasa.


“Ametokea Nairobi, Kenya alipokwenda kuchukua viza ya kuelekea huko, upo uwezekano mkubwa wa kufuzu majaribio hayo,” alisema Gibby.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic