June 24, 2015


Yanga jana imepata ushindi wake wa kwanza kabla ya kuanza msimu mpya wa Ligi Kuu Bara kwa kuifunga Friends Rangers mabao 3-2 huku mshambuliaji mpya, Malimi Busungu akipiga mbili pekee.


Mechi hiyo, ilipigwa kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam iliyoudhuliwa na watazamaji wengi waliofika kuwaangalia nyota wapya waliowasajili kwa ajili ya msimu ujao wa ligi kuu na Ligi ya Mabingwa Afrika.

Katika mchezo, Kocha Mkuu wa Yanga aliwaanzisha  wachezaji watatu pekee wa kikosi cha kwanza ambao ni Kelvin Yondani, Salum Telela na Juma Abdul huku wengine wakiwa wapya waliosajili kwa ajili ya msimu ujao na wa kikosi cha pili.
Wachezaji wapya aliowaanzisha katika mechi hiyo kwa hiyo kuangalia uwezo wao ni Deus Kaseke, Benedicto Tinoco na Lansana Kamara.

Katika mechi hiyo, Yanga ndiyo walikuwa wa kwanza kupata bao la kwanza kupitia kwa Mliberia, Kpah Sherman akiunganisha pasi safi ya Busungu katika dakika 20 ya mchezo huo.

Bao hilo alikudumu muda mrefu baada ya mshambuliaji wa Friends Rangers, Ally Rooney kupiga faulo safi nje ya 18 na kumchambua Tinoco baada ya Kelvin Yondani kumchezea vibaya.

Yanga ilipata bao la pili kupitia kwa Busungu baada ya kugongeana na Sherman kabla ya kumchambua kipa wa Friends Rangers, bao hilo alikudumu baada ya wapinzani kusawazisha kupitia kwa Cosmas Lewis ‘Baloteli’ kwa shuti kali la mita 20 lililomshinda Ally Mustapha ‘Barthez.

Katika dakika ya 87, Busungu akaifungia bao la tatu Yanga akiunganisha krosi safi ya kiungo mshambuliaji Mbrazili, Andrey Coutinho na kufanya mechi hiyo kumalizika kwa Yanga kuibuka kwa ushindi wa mabao 3-2.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic