June 14, 2015


Wakati Tanzania imepoteza mechi yake ya kwanza katika kuwania kucheza Kombe la Mataifa Afrika, timu zote za ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, zimefanya vizuri.


Rwanda ikiwa ugenini chini ya nahodha Haruna Niyonzima imeshinda ugenini kwa bao 1-0 dhidi ya Msumbuji.

Bao hilo moja limeifanya limeiweka Rwanda katika nafasi nzuri ya kufanya vizuri zaidi kuwania kucheza Afcon.

Timu nyingine imefanya vizuri Ethiopia imeshinda kwa mabao 2-1 dhidi ya Lesotho. Kenya nayo ikatoka sare ya bao 1-1 dhidi ya 1-1 ikiwa ugenini dhidi ya Congo.


Sudan ikiwa nyumbani, imeitwanga Sierra Leone kwa bao 1-0 ikiwa jijini Kharthoum huku DR Congo ikiibuka na ushindi wa bao 2-1 dhidi ya Madagascar.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic