Taifa Stars
imeanza vibaya kampeni ya kuwania kucheza Kombe la Mataifa Afrika baada ya
kuchapwa mabao 3-0.
Katika mechi
iliyochezwa jijini Alexandria, Stars imefungwa mabao hayo na wenyeji wake Misri
ndani ya dakika 45. Mabao matatu ya Misri yamefungwa na wachezaji wake nyota akiwemo mshambuliaji wa zamani wa Chelsea, Mohammed Salah.
Hadi mapumziko
timu hizo zilikwenda zikiwa hazijafungana lakini kipindi cha pili kikaonekana
kuwa cha mateso kwa Stars.
Misri ilianza kuandika bao la kwanza katika dakika ya 61 kupitia kwa Rami Rabia kabla ya Basemi Morsi kufunga la pili katika dakika ya 65.
Salah ndiye aliyeikata maini Stars baada ya kufunga bao la tatu katika dakika ya 70. Bao hilo lilionyesha kuimaliza kabisa Stars iliyoweka kambi nchini Ethiopia kabla ya kwenda nchini Misri kwa ajili ya pambano hilo.
Misri ilianza kuandika bao la kwanza katika dakika ya 61 kupitia kwa Rami Rabia kabla ya Basemi Morsi kufunga la pili katika dakika ya 65.
Salah ndiye aliyeikata maini Stars baada ya kufunga bao la tatu katika dakika ya 70. Bao hilo lilionyesha kuimaliza kabisa Stars iliyoweka kambi nchini Ethiopia kabla ya kwenda nchini Misri kwa ajili ya pambano hilo.








0 COMMENTS:
Post a Comment