Timu
ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inayodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro Premium
Lager inaondoka nchini leo jioni kuelekea Kampala - Uganda kwa ajili ya mchezo
wake wa marudiano dhidi ya The Cranes siku ya jumamosi.
Kikosi
cha Taifa Stars kinaondoka kikiwa na wachezaji 20, bechi la ufundi 7, pamoja na
viongozi kwa shirika la ndege la Rwanda (Rwada Airi) ambapo wanatarajiwa
kuwasili uwanja wa Entebe majira ya saa 3 usiku kwa saa za Afrika Mashariki na
Kati.
Mchezo
wa jumamosi ni wa marudiano kuwania kufuzu kwa fainali za Afrika kwa wachezaji
wa ndani (CHAN) zitakazofanyika nchini Rwanda, huku mechi hiyo ikichezwa saa 10
jioni katika uwanja wa Nakivubo.
Kocha
mkuu wa Taifa Stars, Charles Mkwasa amesema vijana wake wamefanya mazoezi
vizuri katika kipindi chote cha maandalizi, na sasa wako tayari kwa mchezo huo,
mipango ikiwa ni kupata ushindi siku ya jumamosi.
Aidha
Mkwasa amesema watawakosa wachezaji wawili, Abdi Banda na Mohamed Hussein
(Tshabalala) waliopata majeruhi jana wakati wa mazoezi yaliyofanyika uwanja wa
Boko Vatereani, na kusema nafasi zao zitazibwa na wachezaji waliopo kambini.
Wachezaji
wanaosafiri ni: Ally Mustafa, Mudathir Khamis, Juma Abdul, Shomari Kapombe,
Haji Mngwali, Michael Aidani, Hassan Isihaka, Kelvin Yondani, Nadir Haroub,
Frank Domayo, Mudathir Yahya, Salum Telela, Said Ndemla, Saimon Msuva, Deus
Kaseke, Ramadhan Singano, Atupele Green, Rashid Mandawa, John Bocco na Ame
Ally.
0 COMMENTS:
Post a Comment