Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa
Miguu nchini (TFF), Mwesigwa Selestine ametuma salamu za rambi rambi kwa famili
aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa TFF, Fredrick Mwakalebela kufuatia kufiwa na baba
yake mzazi jana mjini Irinnga na mazishi yakitarajiwa kufanyika kesho mjini
Iringa.
Aidha, TFF imetuma salam za rambi rambi
kwa kocha mkuu wa timu ya Mbeya City, Juma Mwambusi kufutia kufiwa na mama yake
mzazi mjini Mbeya.
TFF pia imetuma salam za rambi rambi kwa
familia ya mtangazi maarufu wa wa michezo nchini Ezekiel Malongo
aliyefariki dunia jana.
Katika salam zake kwa familia ya
Mwakalebela, Mwambusi na Malongo, Mwesigwa amesema wanawapa sana pole wafiwa
kwa kuondokewa na wapendwa wao na kusema kwa niaba ya TFF, familia ya mpira na
watanzania wote wapo nao pamoja katika kipindi hichi cha maombolezo.
0 COMMENTS:
Post a Comment