July 28, 2015


Mmoja wa makocha wanaoaminika kuwa ni wakali na hawataki mchezo kazini ni Jose Mourinho.


Kocha huyo wa Chelsea amefanya kazi katika nchi za Ureno, England, Italia na Hispania na kote amechukua ubingwa wa nchi.

England amebeba mara mbili, lakini pamoja na ukali wake, bado anaonekana ni mtu anayejua ‘kucheza’ na akili za wachezaji wake.
 
Angalia alivyotengeneza mchezo kama vile wanaoendesha ndege, unaweza ukadhani watoto wanacheza. Walipojisahau, wakamwagiwa barafu ingawa nahodha John Terry anajua michezo ya Mourinho, hivyo alikuwa wa kwanza kutimua mbio.

Mfano kuandaa michezo mbalimbali inayowafanya wacheke sana na kusahau ugumu wa mazoezi au ukali wake.

Michezo hiyo inawafanya wajione ni sehemu ya familia na watu wanaotaka kutimiza lengo moja kwa pamoja.







0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic