July 21, 2015

KMKM
Baada ya kupoteza mchezo wao dhidi ya Gor Mahia, KMKM wanaamini bado wana nafasi ya kufuzu kwenye hatua ya mtoano.


KMKM ilichapwa kwa mabao 3-1 na Gor Mahia ya Kenya ambayo imejihakikishia robo faibnali ya michuano ya Kagame baada ya kushinda mechi ya pili mfululizo.

Kocha Mkuu wa KMKM, Ali Bushir ‘Shilton’ amesema ana imani kubwa na kikosi chake.

“Kuna makosa ambayo tunajifunza, soka ndiyo iko hivyo kuna siku mnafanya vizuri na nyingine mnateleza.
“Uliona tulivyocheza vizuri hasa kipindi cha kwanza, lakini dakika za mwisho tukateleza.

“Imani yangu kubwa tutajirekebisha na kufanya vizuri mechi zilizobaki,” alisema Bushiri.

KMKM ina mechi mbili na pointi tatu kibindoni baada ya kuanza michuano hiyo kwa ushindi halafu ikapoteza mechi ya pili.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic