July 15, 2015


Vyombo vya habari vya Ureno na Hispania vimetoa mpya baada ya kuandika kuwa kipa mpya wa Porto, Iker Casillas kwamba amekutana na adui yake Kocha Jose Mourinho.


Hata hivyo haikuwa kweli kwamba wawili hao walikutana ‘live’ baada ya Casillas kutua Porto.

Casillas alikutana na sanamu la Mourinho ambalo liko kwenye makao makuu ya klabu hiyo katika sehemu maalum ya jumba la kumbukumbu.

Mourinho alipata mafanikio makubwa akiwa FC Porto kabla ya kwenda  England kuinoa Chelsea.


Casillas ambaye hakuwa akielewana na Mourinho walipokuwa Real Madrid, alipokelewa na rais wa Porto, Pinto da Costa na kutembezwa katika sehemu mbalimbali za klabu hiyo ikiwemo kwenye jumba hilo la kumbukumbu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic