July 15, 2015


Licha ya kujishughulisha na sanaa ya Muziki wa Bongo Fleva, Hamis Baba ‘H Baba’, ameamua kujiunga na kikosi cha Toto Afrika ya Mwanza kwa ajili ya kukitumikia msimu ujao wa Ligi Kuu Bara inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi kuanzia Agosti 22, mwaka huu.


H Baba anayemudu nafasi ya ufungaji, tayari ameonekana kujiunga na kikosi hicho huku akiwa anaendelea na mazoezi chini ya kocha John Tegete, ambapo aliongeza kuwa keshokutwa Ijumaa ndiyo anatarajia kumalizana na uongozi wa klabu hiyo pamoja na kusaini mkataba.

H Baba amesema alitakiwa tayari kuwa mmoja wa wachezaji wa timu hiyo lakini kuna mambo flani ambayo bado alikuwa hajayakamilisha.

“Ilikuwa niwe nimeshamalizana na uongozi wa Toto lakini kuna baadhi ya mambo ndiyo yalikuwa hayajakaa sawa ila mpaka Ijumaa nadhani kila kitu kitakuwa sawa.


“Licha ya kutomalizana na uongozi wa timu hiyo, tayari nimeshajiunga na wenzangu ambapo tayari ninaendelea na mazoezi ya kujiandaa na msimu ujao wa ligi kuu chini ya kocha John Tegete,” alisema H Baba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic